Ijumaa, 2 Oktoba 2015

BOND AFUNGUKA MAZITO KUHUSU WASTARA JUMA

 Mcheza filamu za kitanzania na mtangazaji wa kipindi cha action and cut ,Bond bin sinan amesema amesema 27.09.2014 ndio tarehe ambayo mama yake mzazi amefariki dunia,lakini cha kushangaza tarehe hiyo hiyo miaka tofauti mwenyezi mungu amemleta mcheza filamu mwenye jina kubwa nchini Wastara Juma Issa ambae ndio mpenzi wake kwasasa

akifunguka kiafrika bila hofu yoyote Bond ameshindwa kuzuia furaha yake na kuandika mazito kupitia ukurasa wake wa facebook



Siku ya Tarehe 27 mwezi wa 9 mwaka 1994 ni siku Mama yangu alinifariki na kuniacha mpweke na nikajiona kuwa sitakuwa na furaha. 

Lakini tarehe hiyo hiyo 27/09 kasoro mwaka alizaliwa binti mmoja mzuri wa ajabu mwenye sifa nyingi nzuri ambazo kila mtanzania anazijua kuanzia kazi, upendo, huruma, uvumilivu na ujasiri kwakweli mungu hajawahi kukosea wala hatokosea kufanya maamuzi

Kwani humpa amtakae na humnyima amtakae na yote ikiwa ni kwa kheri zake
Asante mungu kwa kunijaalia kunipa na kumjua huyu mwanamke mzuri