Mcheza filamu za kitanzania na mtangazaji wa kipindi cha action and cut ,Bond bin sinan amesema amesema 27.09.2014 ndio tarehe ambayo mama yake mzazi amefariki dunia,lakini cha kushangaza tarehe hiyo hiyo miaka tofauti mwenyezi mungu amemleta mcheza filamu mwenye jina kubwa nchini Wastara Juma Issa ambae ndio mpenzi wake kwasasa
akifunguka kiafrika bila hofu yoyote Bond ameshindwa kuzuia furaha yake na kuandika mazito kupitia ukurasa wake wa facebook
Siku ya Tarehe 27 mwezi wa 9 mwaka 1994 ni siku Mama yangu alinifariki na kuniacha mpweke na nikajiona kuwa sitakuwa na furaha.
Lakini tarehe hiyo hiyo 27/09 kasoro mwaka alizaliwa binti mmoja mzuri wa ajabu mwenye sifa nyingi nzuri ambazo kila mtanzania anazijua kuanzia kazi, upendo, huruma, uvumilivu na ujasiri kwakweli mungu hajawahi kukosea wala hatokosea kufanya maamuzi

